Na Peter Akaro
Malcolm Forbes aliwahi kusema kushindwa ni mafanikio kama tutajifunza kwenye hilo,ni wazi Tanzania kwenye mchezo wa riadha tumeshindwa tena kwa kiasi kikubwa,je tunatambua hilo na kutaka kujirekebisha?,jibu rahisi ni hapana.
Wiki iliyopita mashindano ya riadha ya Kili Marathon yalifanyika mjini Moshi,yalikuwa ni mashindano ya 14 kufanyika,huku tukishudia Wakenya waking’ara katika mashindano hayo kama ilivyo desturi yao.
Ninaposema riadha imesahaulika,nimetumia kigezo cha kawaida tu,kwa kutazama namna mashindano ya Kili Marathon yalivyofanyika.Licha ya kuwa mashindano makubwa yaliyojumusha wanaridha kutoka zaidi ya nchi 45 dunia,bado najiuliza thamani ya mashindano haya kwetu ipo wapi.
Mpaka mashindano haya yanafanyika sikuona wala kusikia yakizungumziwa au kupewa nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari hapa nchini,kama kuna mchezo kati ya Simba na Yanga,basi wiki ya tukio utasikia mashabiki wa timu hizi na viongozi wao wakitambiana kwenye vyombo habari,ilimradi kutengeneza hali ya upekee katika mchezo.
Mbona hili halikufanyika Kili Marathon?,kuanzia kwa viongozi wa riadha,serikali,wadau wa michezo na vyombo vya habari ulikuwa wajibu wao kufanikisha hilo,sikitiko langu ni kwamba Kili Marathon imekuja kimya kimya na kuondoka kimya kimya,lakini ni kweli watanzania hatujui thamani ya mashindano haya?.
Kuna akili ya kitoto inaniambia huenda mzamini na yeye ameshakaitshwa tamaa na mwenendo wa riadha hapa nchini,mzamaini huyu ndo Yule anayedhimini pambano la Simba na Yanga maarufu kama mtani jembe,na utuaji wa tuzo za muziki maarufu kama KTMA,ukiangalia hivi vitu viwili mzamini huvitangaza sana kwenye vyombo vya habari na kwingineko,lakini mbona hafanyi hivyo kwa Kili Marathon?,hilo ni swali la kitoto lililoletwa na akili ya kitoto.
Wakenya ndo wanajua thamani na utamu wa mashindano haya,ndio wanajua,kama mbio za KM 45 kwa wanaume na wanawake medali zote wamechukua wao,na mbio za KM 21 katika zile nafasi 6 za zawadi(kwa wanaume na wanawake) watanzania wawili tu ndo walioambulia,nafasi zote 4 wakachua wao,kwa nini wasijue utamu wa mashindano haya,kama wanaridha zaidi ya 250 wametoka Kenya wakaja kushiriki ni wazi wanajua thamani ya mashindano haya.
Wakati anafunga mashindano hayo waziri mwenye dhamana ya michezo Nape Nnauye aliwashukuru sana waandaji wa mashindano hayo kwani wamesaidia kutangaza utalii wa mlima Kilimanjaro,kwa upande wake alikuwa sahihi akiwa kama kiongozi wa serikali,huenda ndo kitu pekee cha kujivunia kutoka kwenye mashindano hayo kwa wakati huu ni utali,kama kutakuwa na lingine usisite kuniambia.
Lengo kuu la mashindano haya ni kuinua mchezo wa riadha na kuwaleta watu pamoja,ndo maana kuna mbio za kujifurahisha,swala la utali nafikiri linachukua nafasi ya pili,je lengo kuu limefikiwa?,na kama limefikiwa ni kwa asilimia ngapi?,maswali haya yananiacha njia panda.
Baada ya mashindano haya kumalizika viongozi wa riadha nchini wana nini cha kujivunia kwa sasa?,zaidi ya kuandaa,wakati wa kufunga mashindano hayo rais wa shirikisho la riadha Tanzania RT,Anthony Mtaka alimwambia waziri mwenye dhamana ya michezo Nape Nnauye,changamoto kubwa inayowakabili ni matokeo katika mashindano hayo,yaani wanariadha wa Tanzania kutofanya vizuri,huku (akijitetea) wanzentu wanajiandaa sana.
Kwa maana hiyo tunatka kujitete sisi hatukujindaa ndo sababu ya kushindwa,swala maandalizi nani anapaswa kulifanya?,zaidi ya shirikisho na wanaridha wenyewe,kama hiyo haitoshi,hatukufahamu mashindano yako mbioni kufanyika.
Mmoja kati ya washindi kutoka Kenya,alisema Tanzania kuna sehemu nzuri sana kujifunzia(mazoezi) kama mlima Kilimanjaro na sehemu nyingine zenye milima.
“Na kama imekua ngumu tunaomba mamlaka ya uamiaji Tanzania kwa sababu ni ndugu zetu,watume wanariadha waje kujifunza Kenya kwenye maeneo tofauti,wengine wajifunze Meru,wengine Kenya Uguru,na wakienda ng`ambo watakuwa wakimbiaji wazuri” alisema mshindi huyo.
Huenda hawa mwenzetu wanatushangaa kwa nini hatufanyi vizuri wakati tuna kila kitu!!!!.Na mashindano yakawa yameishia hapo,Wakenya wakapanda ndege kurejea kwao na medali kibao