GWAJIMA AACHIWA KWA DHAMANA

 Askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Joseph Gwajima aliyekuwa amelazwa katika hospitali ya TMJ ya jijini Dar es saalam baada ya kuugua ghafla wakati akifanyiwa mahojiano na jeshi la polisi,ameachiwa kwa dhamana na jeshi hilo huku akitakiwa kufika katika kituo kikuu cha polisi april 02,2015 kwa ajili ya kuendelea na mahojiano na jeshi la polisi.


Taarifa za awali zilikuwa zinasema kwamba askofu Gwajima angefikishwa kituo kikuu cha polisi jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuendelea kuhojiwa na jeshi la polisi kutokana na kusitishwa kwa mahojiano hayo baada ya kuugua ghafla na kulazwa katika hospitali ya TMJ jambo ambalo lilisababisha wafuasi wake kuanza kukusanyika kituoni hapo huku askari polisi wakitumia nguvu ya ziada ya kidiplomasia kuwatawanya.



Hata hivyo majira ya saa saba za mchana kukawepo na taarifa mpya za askofu Gwajima kufikishwa katika kituo cha polisi cha Osterbey kilichopo katika mkoa wa kipolisi wa kinondoni na kushuhudia umati mkubwa wa askofu huyo ukiwa nje ya kituo hicho huku baadhi ya askari wa kituo hicho wakiwa na silaha wakiranda randa katika eneo zima la kituo hicho wakati askofu huyo akiwa ndani ya kituo hicho cha polisi.


Haikuweza kufahamika mara moja kwa wandishi wa habari sababu za askofu Gwajima kufikishwa kituoni hapo ni kuendelea na mahojiano ama la hadi baadae ambapo taarifa zikatoka kwamba amefikishwa kituoni hapo kwa ajili ya dhamana kutokana na kuruhusiwa kutoka hospitalini baada ya afya kuimarika.








No comments: