WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUWA WABUNIFU

Mwandishi  Eva Mbesele (TSJ).
Waandishi wa habari hususani ambao bado wapo vyuoni wametakiwa kuwa wabunifu pamoja na kuiheshimu taaluma yao ili waweze kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye soko la ajira katika  sekta ya habari ambayo inakua kwa kasi hapa nchini. 


Geti kubwa la kuingia kwenye ofisi za shirika la utangazaji Tanzania TBC zilizopo Bamaga jijini Dar es salaam


Wito huo umetolewa leo na Angela Man’genya ambae ni mhariri 
wa habari za Redio katika shirika la utangazaji Tanzania TBC wakati akizungumza na wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Time School of Journalism  (TSJ) walipotembelea ofisi za   shirika hilo zilizopo Bamaga jijini Dar es salaam kwa  ziara ya kimasomo
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha uandishi wa habari (TSJ) wakiwa mapokezi wakisubiri utaratibu wa kuingia kwenye ofisi za TBC kwaaji ya ziara ya kimasomo
 
Aidha  Man’genya aliongeza kuwa wanahabari ambao bado wapo vyuoni wanatakiwa kusoma kwa bidii na sio kwenda chuo kuonyeshana ufahari wa mavazi kwani tasnia ya habari inakua kwa kasi sana na inahitaji watu ambao wamesonma.

“Waandishi wa habari  mnatakiwa kuwa wabunifu na kujituma  sio kusubiri mpaka upanangiwe kazi” Alisema Man’genya.


 Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari (TSJ) wakiingia kwenye ofisi za shirika la utangazaji Tanzania TBC

Katika ziara hiyo wanafunzi hao walijifunza vitu vingi ikiwemo jinsi ya kuandaa habari, kusoma habari, kuhariri vipindi vya Radio pamoja na Luninga napia walitembelea sehemu mbalimbali ndani ya ofisi za shirika hilo zikiwemo chumba cha kufanyia vipindi mbalimbali, chumba cha kupokelea matangazo ya nje, chumba cha kuhariri habari na chumba cha kusomea taarifa za habari.

 Baadhi ya wanafunzi wa (TSJ) wakiwa kwenye studio ya kufanyia vipindi kwenye ofisi zashirika la utangazaji Tanzania TBC




 Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari (TSJ) wakipata maelekezo kwenye chumba cha habari cha TBC


























Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari (TSJ) wakiwa kwnye chumba cha kurushia matangazo ya television kwenye ofisi za shirika la utangazaji (TBC)



 Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari (TSJ) wakiwa kwenye chumba maalumu cha kusomea taarifa za habari  katika ofisi za shirika la utangazaji Tanzania TBC

 






 

No comments: