10 WAFIKISHWA MAHAKAMANI VURUGU ZA MAPANGONI TANGA

WAKAZI 10 wa jijini Tanga, akiwemo mwanafunzi wa sekondari wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wakikabiliwa na makosa matano tofauti kuhusu tukio la kuwanyang’anya polisi silaha pamoja na kumuua askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Sajenti Mohamed Rashid Kajembe.




Mwanafunzi aliyefikishwa mahakamani ni Rajab Bakari (19) wa shule ya sekondari na mkazi wa Makorora jijini hapa.

Watuhumiwa tisa wameelezwa kuwa ni wafanyabiashara, nao ni Mbega Seif (25) maarufu ‘Abuu Rajab’ mkazi wa Kiomoni, Amboni, Ayubu Ramadhani (27) maarufu ‘Chiti’ ambaye ni fundi umeme na mkazi wa Kona Z Kiomoni, Hassani Mbogo (20) maarufu ‘Mpalestina’ mkazi wa Makorora, Mohamed Ramadhani (19) mfanyabiashara na mkazi wa Makorora, Sadiki Mdoe (25) maarufu ‘Kizota au Kisaka’ mkazi Magaoni.
 
Washtakiwa wengine ni Saidi Omari (26) mkazi wa Magaoni Tairi Tatu, Nurdin Mbogo (27) Makorora, Ramadhan Mohamed (18) mkazi wa Donge pamoja na Omari Harubu Abdala (55) maarufu ‘Ami’ 


Wakisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Aziza Rutala, Wakili wa Serikali, George Barasa akisaidiana na MariaClara Mtengule, walidai kuwa kosa la kwanza hadi la tatu linawahusisha washitakiwa namba moja mpaka nane (1 -8) ambao wanatuhumiwa kushiriki kula njama ya kutenda kosa kinyume cha sheria.

No comments: