IDODI SEKONDARI YAFUNGWA

Serikali wilayani IRINGA imeifunga shule ya Sekondari ya IDODI iliyopo Tarafa ya Idodi kwa muda wa wiki mbili ili kutoa nafasi ya kufanyika ukarabati na uchunguzi wa mfululizo wa matukio ya kuungua moto kwa mabweni ya shule hiyo. 


Tangazo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Angelina Mabula kufuatia tukio la kuungua moto kwa bweni jingine la wasichana la shule hiyo hapo jana ikiwa ni tukio la pili ndani ya mwezi mmoja. 



Mkuu wa wilaya hiyo Angelina Mabula ametembelea shule hiyo kujionea hali halisi huku akiwafariji wazazi na wanafunzi walioathirika na moto na kutoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano. 



Mkuu wa Shule ya Idodi, Mwalimu Christopher Mwasomola anasema agizo la kufanya mabadiliko ya mfumo wa umeme yalifanyika lakini hayajazaa matunda. 



Moto huo umezua Taharuki kubwa kwa Wanafunzi na Wazazi na baadhi wakihusisha na imani potofu na kutoa mapendekezo kwa serikali ikiwemo kuangalia iwapo wananchi waliokuwa wanakaa eneo hilo kabla ya kuwa shule wali ridhia kuondoka katika eneo hilo. 



Hii itakuwa ni mara ya tatu kwa mabweni ya Shule ya idodi kuungua baada ya tukio la moto la mwaka 2009 lililogharimu maisha ya wanafunzi 12.







No comments: