IFAHAMU ISHARA KUU YA TAIFA LA CHINA


 China ni nchi yenye historia ndefu na utamaduni mkukbwa, na vivutio vingi vya utalii. Kumbukumbu nyingi za mandhari ya kimaumbile na za utamaduni zinadhihirisha akili nyingi na juhudi kubwa za watu wa China ya kale. Mwaka 1985 serikali ya China ilijiunga na “Mkataba wa Urithi wa Dunia”, na mwaka 1987, kumbukumbu 6 za urithi wa China ikiwa ni pamoja na Ukuta Mkuu na Kasri ya Kifalme ya China viliwekwa kwenye orodha ya urithi wa dunia. 


 Ukuta Mkuu unasifiwa kama ni “moja katika maajabu 7 ya dunia” ni jengo kubwa ambalo lilitumia miaka mingi na kazi kubwa duniani, katika ngome zote za kuzuia maadui katika zama za kale. Ukuta huo una urefu wa zaidi ya kilomita 7,000.


Historia ya ujenzi wa ukuta huo inaweza kufuatiliwa hadi karne ya 9 kabla ya Kristo. Katika kipindi cha “Madola Kivita” kilichokuwa kati ya mwaka 770 K.K. na 476 K.K. madola yalikuwa yakipigana vita na kila moja likitaka kuliangamiza lingine ili kupata utawala wa China nzima, kutokana na sababu hiyo kila dola lilijenga ukuta milimani kwenye mipaka ili kuzuia mashambulizi ya maadui. Mwaka 221 kabla ya Kristo, mfalme Qin Shuhuang aliiunganisha China nzima, kisha akaziunganisha kuta zote zilizojengwa na madola hapo awali na zikawa ukuta mkuu. Katika miaka zaidi ya elfu mbili kila enzi ilizidi kuongeza urefu wa kuufanya ukuta huo kuwa na kilomita elfu 50, urefu ambao unaweza kuizunguka dunia kwa duara na zaidi kwa kufuata ikweta. 

Kwa kweli Ukuta Mkuu umelowa jasho na damu za wahenga wa China na pia ni matokeo ya akili za mababu wa China. Ukuta huo umepita miaka zaidi ya elfu moja bila kuanguka, sifa zake haijapotea, umekuwa ni ishara ya taifa la China. Mwaka 1987 ukuta huo uliorodheshwa kwenye urithi wa dunia kwa jina la “ishara ya taifa la China”.










No comments: