2015 HIYOOOOOO...!! INAONDOKA, TUTAIKUMBIKA KWA HAYA KIMICHEZO



Kuna msemo wa kiswahili unaosema, hakuna lenye mwanzo linalokosa  mwisho, zimebaki siku chache ili mwaka 2015 uweze kufika mwisho na hatimaye kuukaribisha mwaka mpya wa 2016.

Mwaka 2015 umekuwa wa kihistoria kwenye nchi ya Tanzania, kwavile ulisheheni matukio mbalimbali ya kufurahisha pamoja na kusikiktihsa,matukio ya kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni pamoja na kimichezo yaliweza kujitokeza hapa nchini.

Tukiwa tunaelekea kuumaliza mwaka 2015 na kuukaribisha mwaka 2016, makala hii inakuletea matukio mbalimbali ya kimichezo yaliyojitokeza mwaka huu na kuteka hisia za  wanamichazo wengi nchini Tanzania.

Kichapo cha magoli 7-0 ilichokipata Tanzania dhidi ya Algeria
Baada ya kufanikiwa kuitoa timu aya taifa ya Malawi kwa ushindi wa jumla wa mabo 2-1, kwenye mechi ya raundi ya kwanza kufuzu hatua ya makundi, kuwania tiketi ya kushiriki fainali za kombe la Dunia zinazotarajiwa kufanyika mwaka 2018 nchini Urusi, timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ilikutana na timu ya taifa ya Algeria.
Kwenye mechi ya kwanza iliyopigwa kwnye uwanja wa taifa jjini Dar es salaam, timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2, mabao ya stars yakifungwa na Elias Maguri na Mbwana Samata, huku yale ya kusawazisha ya Algeria yakifungwa na Islam Sliman.
Wiki moja baadae Stars walisafiri kwenda nchini Algeria kucheza mechi ya marudiano na mbweha hao wa jangwani, na kushuhudia stars




wakipokea kipigo cha fedheha cha bao 7-0. Kwa matokea hayo Stars ilisukumizwa nje ya mashindano hayo kwa jumla ya mabao 9-2.
Matokeo hayo yaliwashtua sana wapenzi wengi wa soka hapa nchini kutokana na kiwango walichokionyesha Stars kwenye mechin ya kwanza hapa nyumbani.
“Kwakweli sikutegemea tungefungwa idadi hiyo ya mabao, kwa jinsi timu ilivyocheza mechi ya kwanza hapa nyumbani , wachezaji walionyesha kujituma na kujiamini sana na kutawala mchezo vizuri. Lakini ndio mpira jinsi ulivyo kilichobaki ni kuangalia mashindano mengine,” aliseama Frank William shabaiki wa soka kutoka maeneo ya kinondoni.

Kukamilika kwa mradi wa kituo cha michezo cha Jakaya Kikwete Youth Park.
Mwezi Oktoba mwaka huu aliyekuwa Rais wa awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete alizindua kituo cha michezo cha Jakaya Kikwete Youth Park kilichopo eneo la kidongo chekundu jijini Dar es salaam, kilichojengwa na kampuni ya umeme ya Symbion Power kwa kushirikiana na klabu ya Sunderland inayoshiriki ligi kuu ya England.

Dk Kikwete alikubali kuzindua kituo hicho wakati wa mazungumzo kati yake na mtendaji mkuu wa Symbion Power, Paul Hinks kwenye hotel ya JW Marriot Essex House mjini New York nchini Marekani, ambako Rais huyo mstaafu alipokuwa anafanya ziara ya kikazi nchini humo.



Hinks alimueleza Dk kikwete kuwa ujenzi wa kituo hicho umekamilika tayari kwa uzinduzi na hivyo kuongeza thamani kubwa kwenye eneo ambalo zamani lilkua gereji ya kutengeneza magari.

Kituo hicho kimegharimu kiasi cha Dola za kimarekani milioni mbili na ni matokeo ya ushirikiano wa kampuni ya Symbion Power ya Marekani, klabu ya soka ya Sunderland inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza na taasisi ya Grasshopeper Soccer ya nchini Australia.


Kituo hicho kitatumika kuendeleza vipaji kwa vijana wenye umri chini ya miaka 10 katika michezo  kama mpira wa miguu, mpira wa magongo pamoja na kakapu.

Samata, Ulimwengu waweka rekodi
Nyota wa kimataifa wa Tanzania mbwana Samata, alifunga goli moja kwenye ushindi wa magoli 2-0, iliyoupata timu yake na Tp Mazembe kwenye mchezo wa marudiano wa fainali ya klabu bingwa Afrika dhidi ya Usm Alger, mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Stade TP Mazembe mjini Lubumbashi, Jamhuri ya Kdemikrasia ya Kongo.

Goli hilo lilimfanya Samata kuwa mfungaji bora wa mashindano hayo kwa kufikisha jumla ya magoli 8, akimpiku Bakryu’Al Medina wa El Merekh  aliyefunga jumla ya magoli 7 ambaye alikua akichuana nae kwa karibu.
Samata na Ulimwengu wameweka rekodi ya kuwa watanzania wa kwanza kunyanyua kombe la klabu bingwa Afrika, huku nyota wengine waliong’ara kwenye medani ya soka wakishindwa kufanya hivyo.

Kwa upande wake Samata ameweka rekodi ya kuwa mtanzania wa kwanza kunyakuwa tuzo ya mfungaji bora wa michuano ya klabu bingwa Afrika.
Wachezaji hao pia wameweka rekodi ya kuwa watanzania wa kwanza kucheza michuano ya klabu bingwa ya dunia yanayoendelea nchini Japani.

Azam yaweka rekodi kombe la Kagame
Azam Fc iliwatoa kimasomaso watanzania baada ya kufanikiwa kutwaa kombe la klabu bingwa Afrika mashariki na kati (Kagame) kwa kuilaza timu ya Gor mahia ya Kenya kwa mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa.

Ubingwa huo  wa Kagame ni wakwanza kwenye historia ya klabu hiyo baada ya kufanikiwa kuchjeza fainali mbili, fainali ya kwanza walicheza mwaka 2012 dhidi ya klabu ya Yangana kupoteza kwa magoli 2-0, na mwka huu wameingia katik historia ya vilabu vilivyofanikiwa kulitwaa kombe hilo.

Kitu cha kufurahisha na chakukumbukwa katika michuano hiyo ni baada ya Azam kutwaa ubingwa huo bila Kurusu wavu wao kuguswa, ukiacha magoli matatu waliyofungwa na Yanga wakati ikitoka na ushindi wa matuta 5-3 kwenye hatua ya robo fainali.

Kwa ubingwa huo klabu hiyo ilifanikiwa kuondoka na kitita cha Dol za kimarekani elfu 40, mshindi wa pili timu ya Gor mahia ilipata Dola elfu 25 na mshindi wa tatu klabu ya KCCA ya Uganda ikipata Dola za kimarekani elfu 10.

Vodacom wasaini mkataba mpya na TFF kwaajili ya udhamini wa ligi kuu bara
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF mwaka huu lilisaini mkataba mpya wa miaka mitatu na kampuni ya simu za mikonni ya Vodacom kwaajili ya udhamnini wa ligi kuu Tanzania bara.

Mkurugenzi wa mawasiliano na masoko wa Vodacom Kelvin Twise alisema mkataba huo unaongezeko la aslimia 40 kutoka kwenye udhamini wa miaka iliyopita ambapo udhamini ulikuwa ni Tshs 1.6 bilioni na mkataba wa sasa utagharimu Tshs 2.3 bilioni.

Twise aliongeza kuwa ongezeko kubwa la udhamini limekwenda katika usafiri wa timu kwa sababu timu nyingi zimekuwa zikilalamika kuwa zinapata wakati mgumu kwenye gharama za usafiri, kwahiyo katika fedha hiyo ya udhamini kiasi cha Tshs 1.2 bilioni zitakwenda kwenye timu zote 16, waamuzi wanagharimu zaidi ya milioni 360, maafisa wengine wa mechi ambao wanakuwa nje ya uwanja  wanagharimu zaidi ya milioni 62,TFF wanapata milioni 183 na zawadi zitagharimu milioni 174.

Ziara ya magwiji wa klabu ya Barcelona .
Mashabiki wa soka nchini mwaka huu walipata nafasi ya kuwashuhudia magwiji wa klabu kubwa Duniani ya FC Barcelona ya nchini Hispania wakiwemo PatrickKluivert, Gazka Mendieta, Anderson De Souza maarufu kama Deco, Francesco Cocu na Luis Garcia walipofanya ziara ya kimichezo mapema mwka huu.

Kwenye ziara hiyo magwiji hao walifanikiwa kutembelea maeneo mbalimbali ya kitalii nchini na kupata nafasi ya kucheza mechi ya kirafiki na magwiji wa Tanzania mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Hii ilikuwa ni mara ya pili kwa magwiji wa klabu kubwa za nchini Hispania kufanya ziara nchini baada ya magwiji wa klabu ya Real Madrid kufanya ziara kama hiyo mwaka uliopita.

Kikosi cha magwiji hao wa Barcelona kilisheheni wachezaji wengi waliotamba kipindi cha nyuma, mbali na Kluivert na wengine ambao mashabiki wengi walikuwa na shauku ya kuwaona pia walikuwepo magwiji wengine waliokuja kwnye zira hiyo chini ya kocha maarufu na kiungo nyota wa zamani wa klabu hiyo mholanzi Johan Cruyff.

Ziara hiyo ilikua na manufaa makubwa kwa nchi ya Tanzania katika Nyanja tofauti kama vile utalii,biashara pamoja na kuanziahsa mahusiano ya kimichezo baina ya klabu hiyo na Tanzania, uhusiano ambao utafungua milango kwa watanzania wenye vipaji vya soka kuapata nafasi ya kwenda kufanya majaribia kwenye klabu hiyo.

Startimes, Sahara Media  wadhamini ligi daraja la kwanza Tanzania bara.
Kapuni ya Startime ilisaini mktaba wa mika mitatu n shirikisho la soka Tanzania (TFF), kwaajili ya udhamini wa ligi daraja la kwanza Tanzania bara wenye thamani ya Tshs milioni 900.

Akizungumza jijini Dar es salaam wakati wa kusaini kataba huo, mkurugenzi  wa Startimes, Langfang Liao alisema lengo la kudhamini ligi hiyo ni kusaidia kuendeleza soka la Tnzania liweze kufahamika na kuonekena moja kwa moj katika chaneli za startimes barani Afrika.


TFF pia iliingia mktaba na kampuni ya Sahara Media Group kupitia chaneli yake ya Star TV wenye thamani ya shilingi milioni 450, kwaajili ya kurusha matangazo ya ligi hiyo nchni.
Udhamini wa kampuni hizo utasaidia ligi hiyo kupunguza changamoto zianazoikabili kama vile vilabu vya ligi hiyo kukosea pesa za usafiri pamoja na malipo ya wachezaji.

Mkwasa apewa shavu Stars
Juni 23 mwaka huu shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF  lilimpatia mkataba wa mwaka mmoja  na nusu kuanzia Oktoba mosi 2015  na kumalizika Machi 31 ,2017 kocha  wa sasa wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa stars) Charles Boniface Mkwasa kukinoa kikosi hicho.

TFF ilifikia makubaliano hayo na Mkwasa baada ya kuridhika na utendji wake katika kukinoa kikosi hicho kama kocha wa muda, ambapo mpaka kipindi hicho alifanikiwa kuiongoza Stars katiaka michezo miwili dhidi ya Uganda na Nigeria ambayo yote iliisha kwa sare.

Hatua hiyo ilikuja baada ya TFF kusitisha mkataba wake na aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo Mholanzi Martin Noij baada ya kutoridhishwa na wa timu apmojana matokeo, ikiwemo kupoteza michezo mitatu ya Cosafa dhidi ya Swatziland, Madagascan a Lesotho pamoja na mchezo wa kuwania kufuzu faianali za AFCON dhidi ya Misri.

Mkwasa ambae kabla kupewa kazi ya kuionoa Stars alikua kocha msaidzi wa klabu ya Yanga, anakuwa kocha wa kwanza mzawa ndani ya kipindi cha zaidi ya miakani 10 iliyopita kupatiwa mkataba wa kuwa kocha mkuu wa kikosi cha timu ya Taifa, baada ya kushuhudia makocha wa kigeni wakina,Marcio Maximo,Kim Poulsen na Martin Noij wakifundisha bila mfanikio yaliyokusudiwa.

Matumla(Junior), amtandika mchina
Mwaka huu bondia wa Tanzania Mohamed Matumla (Snake Jonior), aliwakosha wapenzi wa mchezo wa masumbwi waliohudhuria mpambno mkali na wakusisimua ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee baada ya kumshinda kwa pointi bondia kutoka China Wan Xin Hua, kwenye pambano la raundi 10 Machi 28 mwka huu.

Baadhi ya mashabiki waliojitokeza kwenye usiku huo maalumu uliopewa jina la ‘Night of Knockout’ kushuhudia mpambano huo, wakiwemo wasanii kutoka tasnia mbalimbali hapa nchini pamoja na wapenzi wengine wa mchezo huo, walielezea uzuri wa pambano hilo ambalo lilivuta hisia za wanamichezo wengi hapa nchini hususani wapenda masumbwi.

“Mimi binafsi sijawahi kuhudhuria mapambano ya ngumi, lakini leo nafikiri ndio itakuwa muendelezo wa kuhudhuria mapambano kama haya, kiukweli nimefurahi sana sjawahi kuamini kama kuna mtu anaweza akapigwa hadi akalala chini na kuendelea tena, ila leo nimejionea mwenyewe “,alisema Shetta msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini alipohojiwa na waandishi wa habari mara baada ya pambano hilo.

Simba yavunja mwiko Mkwakwani
Klabu ya wekundu wa msimbazi Simba kwa mara ya kwanza ilifanikiwa kuvuna pointi 6 kwenye dimba la mkwakwani Jijini Tanga baada ya kufanikiwa kupata ushindi kwenye mechi mbili mfululizo katiaka uwanja huo.

Mabingwa hao wa zamani wa ligi kuu  Tanzania bara, walivunja mwiko huo baada ya kuzifunga timu za Afrikani sports 1-0 na Mgambo JKT kwa jumla ya mabao 2-0.

Simba vs Mgambo
Toka klabu ya Mgambo JKT ipande ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013 imekutana na Simba mara 4.
Imeshinda mara 1, imefungwa mara mbili na kutoa suluhu mara 1.
Oktoba 21 mwaka 2012 uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga, Mgambo JKT ilitoka suluhu (0-0) na Simba. Mechi ya marudiano uwanja wa Taifa, Dar es salaam, Mei 8, 2013, Simba ikashinda 1-0.

Msimu uliofuata (2013/2014) Simba chini ya Abdallah Kibadeni, septemba 18 mwaka 2013 iliishindilia Mgambo JKT 6-0 Uwanja wa Taifa Dar es salaam. Mechi ya marudiano Mkwakwani Tanga, Mgambo ikashinda 1-0 na ilikuwa februari 9 mwaka 2014.

Matukio ya Juma Nyosso.
Kwa mashabiki wa soka nchini waliofuatilia ligi kuu bara msimu wa 2014/15 wataendelea kukumbuka tukio la udhalilishaji lililofanywa na beki mahiri wa klabu ya Mbeya city inayoshiriki ligi hiyo  Juma said Nyosso.
Nyosso alimshika makalio, aliyekuwa mshambuliaji wa Simba Elias Maguri wakati wa mechi ya ligi hiyo baina ya Mbeya city dhidi ya Simba, baada ya tukio lile Nyosso aliomba radhi kwa kamati ya maadili ya TFF na kuahidi kuwa hatorudia tena kufanya hivyo.


Mwaka huu kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2015/16 kati timu yake dhidi ya Azam FC Nyosso alirudia tukio lilelile kwa mshambuliaji na nahodha wa klabu ya Azam John Bokko.

Tukio hilo lilionekana kuwachukiza wapenda soka wengi hapa nchini hususani wanaofuatilia ligi kuu bara ukizingatia kuwa alishaahidi kuwa hataruidia kufanya tena .


“Kitendo kilichofanywa na Juma Nyoso ni cha kulaaniwa na kupigwa vita kwasababu kinaharibu maana halisi ya mchezo wa soka ambao ni wa kistaarabu unaochezwa na waungwana wapenda amani lakini kwa beki huyu wa Mbeya City haiko hivyo,” alisema Kheri Mlangwa shabiki wa soka kutoka Temeke.

Baada ya tukio hilo kamati  ya uendeshaji wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania,ilitangaza kumfungia kwa miaka miwili na faini ya Sh. Milioni 2,Nahodha huyo wa Mbeya City kwa kitendo hicho cha udhalilishaji.

No comments: