MAGEREZA WAPEWA SOMO



Watumishi wa jeshi la magereza nchini wametakiwa kufanya kazi kwa weledi ili kuongeza tija na kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli.

Wito huo umetolewa jana na Naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi Mh John Mngodo wakati akifungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa jeshi la hilo nchini.

“Ni lazima kil mmoja afanye kazi kwa bidii na weledi  katika eneno lake ili kuongeza tija, kuboresha sekta ya utumishi wa umma ili kuendana na kasi aliyoanza nayo Rais wa serikali ya awamu ya tano,”alisema

Pia Mngodo alisema kuwa ni muhimu kwa watumishi wa jeshi hilo kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, utunzaji wa mali za serikali na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili fedha zitakazookolewa zitumike katika maeneo mengine ya kimaendeleo.

Aidha ni  lazima kila mtumishi wa umma hususani jeshi la magereza  kuzingatia maadili ya kazi na kuacha kuomba wala kupokea rushwa ili kuendana na dhamira ya Rais Magufulu ya ‘Tanzania bila rushwa inawezekana’.

Awali katika hotuba yake ya kumkaribisha mgeni rasmi Kamishina Jenerali wa Magereza John Minja alisema kuwa kikao hicho kina lengo la kupokea taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya jeshi hilo katika kipindi cha mwaka wa fedha kuanzia Julai hadi Septemba mwaka huu.

Aidha kwa kuzingatia kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano kikao hicho  kitatoa nafasi kwa wajumbe wa baraza hilo kutoa mapendekezo ambayo yatafanyiwa kazi na jeshi la magereza ili kuongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya jeshi hilo.

No comments: