7 WAFARIKI DUNIA KUTOKANA NA MVUA ZINAZOENDELEA NCHINI.

Watu saba wameripotiwa kufariki Dunia  jijini Dar es salaam kutokana na mvua  za masika zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbailimbali nchini.



Wawili kati ya watu waliofariki vifo vyao vimetokana na kukanyaga nyaya za umeme ambazo zilikua kwenye maji baada ya kuanguka kwa nguzo ya umeme  na wengine wamefariki kutokana na kuzidiwa na nguvu ya maji katika eneo la Buguruni kwa myamani jijini Dar es salaam.



Hii sio mara ya kwanza kwa mvua za masika kusababisha vifo vya watu kwani takribani miaka miwili ilopita mvua hizo zimekuwa zikisababisha maafa makubwa ikiwemo vifo pamoja na kuwaacha watu wakiwa hawana mahali pakuishi.

No comments: