WIZI WA MTANDAO WAZUNGUMZWA SANA KWENYE MUSWADA WA SHERIA YA MFUMO WA MALIPO YA MWAKA 2015

Serekali kupitia Waziri wa fedha Mh Saada Mkuya leo imewasilisha bungeni muswada wa sheria ya mfumo wa malipo ya mwaka 2015 huku wabunge wengi wakizungumzia swala la wizi wa mtandao kua ni changamoto na tatizo kubwa katika swala zima la malipo ya kimtandao



Waziri wa fedha Mh Saada Mkuya

Wakichangia katika muswada huo mapema leo jioni baadhi ya wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania wamesema kuwa wizi wa mtandao ni swala lilnalotakiwa kupewa kipaumbele katika muswada huo kwani limekuwa likiwatesa sana wananchi.





Muswada huu  utakuwa ni muswada wa nane kuwasilishwa na serekali katika bunge  hili la kumi baada ya  Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Ajira za Wageni wa Mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Kudhibiti Silaha wa Mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji wa Mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Kodi wa Mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Takwimu wa Mwaka 2014, Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa wa Mwaka 2014 na Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Stakabadhi Ghalani wa Mwaka 2014,



No comments: