AISHI NA WATOTO ZAIDI YA 15 KINYUME CHA SHERIA

Mkazi mmoja wa Moshi mkoani Kilimanjaro Abedi Abdullahi  amekutwa akiiishi na watoto wapatao kumi na saba akiwa amewahifadhi kinyume cha sheria katika nyumba yake kwa madai kuwa anawafundisha elimu ya dini ya kiislam. 

Akizungumzia jinsi anavyoishi na watoto hao Abedi Abdullahi amesema asilimia kubwa ya watoto hao ni ndugu kutoka familia mbalimbali ikiwemo kutoka Moshi na Mwanza na kwamba anawafundisha elimu ya dini ya kiislamu ambapo wazazi wa watoto hao wameridhia jambo hilo. 

Mkuu wa wilaya ya Moshi, Novatus Makunga

Mkuu wa wilaya ya Moshi Novatus Makunga amesema kwa sasa watoto hao wameondolewa katika eneo hilo na kurudishwa kwa wazazi wao huku mahojiano na uchunguzi zaidi wa tukio hilo ukiendelea. 
Ramadhani Mohamed ni mkazi wa Matindigani ambaye ni mmoja wa wazazi wa watoto watatu kati ya hao ambapo amedai kupotelewa na watoto wake tangu februari mwaka jana


No comments: