Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abasi Kandoro na mkuu wa mkoa wa Rukwa mhandisi Stella Manyanya wamemtembelea mtoto Baraka Cosmas ambae ni mlemavu wa ngozi aliekatwa kiganja cha mkono na watu wasiojulikana nyumbani kwao juzi
Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa kanda ya Mbeya, Dk. Mpoki
Ulisubisya akiwaongozwa Wakuu wa Mikoa ya Mbeya na Rukwa kuelekea Wodini
kumjulia hali Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu
wasiojulikana kijijini kwao juzi.
Mtoto
huyo mkazi katika kijiji cha Ikonda kata ya Chitepa wilaya ya Sumbawanga mkoani
Rukwa alihamishiwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kukatwa kiganja
chake akitokea kituo cha Afya cha Kamsamba wilayani Momba mkoani hapa.
Wakuu wa Mikoa ya Mbeya na Rukwa wakimjulia hali Mtoto Baraka
aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu wasiojulikana kijijini kwao juzi.
Akizungumza
kwa masikitiko makubwa mama wa mtoto huyo, Prisca Shaban(28) alisema tukio hilo
lilitokea juzi majira ya saa saba usiku alipokuwa anarudi ndani akitokea nje
kujisaidia alivamiwa na mtu ambaye hakumfahamu na kisha akamsukumia ndani kabla
ya kumpiga kichwani kwa rungu na kisha kupoteza fahamu.
Mama mzazi wa mtoto Baraka,Prisca Shabani akiwa na jeraha kichwani
baada ya kupigwa na watu waliomkata kiganja mtoto wake.
Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa
kulia na watu wasiojulikana kijijini kwao juzi akiwa amelala kitandani
akiendelea kupatiwa matibabu.
No comments:
Post a Comment