Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete jana, Alhamisi, Machi 12, 2015, aliwatembelea na kuwapa pole wahanga wa mvua iliyoandamana na mawe na kusababisha
upotevu wa maisha ya watu na uharibifu mkubwa wa mali katika vijiji
vitatu vya Kata ya Mwakata, Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
Rais Kikwete amewasili mjini Kahama kiasi cha saa nane mchana
baada ya ndege yake kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Mgodi wa Buzwagi na
kwa muda wa kiasi cha saa tatu ametembelea familia ambazo zimepata
madhara makubwa zaidi kutokana na mvua hiyo iliyonyesha kwa kiasi cha
saa moja tu kuanzia saa nne usiku Machi 3, mwaka huu, 2015 na kuambana
na upepo mkali na mawe.
Watu 47 walipoteza maisha, 112 waliumia, nyumba 657 zikabomolewa na kuharibiwa na kaya 468 kuathirika katika vijiji vitatu vya Kata ya
Mwakata na tokea siku ya maafa, Serikali imetoa huduma za dharura za
chakula, sehemu za kulala, huduma za afya na huduma nyingine muhimu kwa
binadamu.
Rais Kikwete ataondoka leo, Ijumaa, Machi 13, 2015, kurejea
Dar es Salaam baada ya ziara hiyo maalum ya siku mbili katika Mkoa wa
Shinyanga.






No comments:
Post a Comment