VIWANGO VYA KODI YA ARDHI KUPUNGUA

Wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi imepanga kuwasilisha kwenye bajeti ijayo mpango maalum wa kupunguza kwa kiasi kikubwa viwango vya kodi ya ardhi ili iweze kulipika na kuwawezesha watanzania walio wengi, wawekezaji na mashirika likiwemo shirika la nyumba la taifa NHC kumiliki ardhi.






















Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh William Lukuvi

Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi, william lukuvi akiongea jijini mwanza na kamati ya kudumu ya bunge ya ardhi maliasili na mazingira kwenye mkutano wa majumuisho ya ziara zilizofanywa na kamati hiyo katika nchi mbalimbali ikiwemo dubai, afrika kusini, uganda na ethiopia amesema serikali pia 
imejipanga kuhakikisha usimamizi na umilikaji wa masuala ya ardhi kuwa wa kielektroniki katika nyanja zote na kuondokana na mfumo wa kizamani wa analog.

Aidha waziri Lukivi amewatoa hofu wananchi wa mji wa kigamboni na amesema serikali haitanyang’anya ardhi wananchi wa mji huo na wala haitawalipa fidia badala yake wananchi watakuwa na haki ya kuyaendeleza maeneo yao wenye au kuingia ubia na wawekezaji kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa au MASTER PLAN ambayo haitasabaisha kero na usmbufu kwa wananchi



































Mji wa kigamboni

Wakiongea kwenye mkutano huo wa majumuisho,baadhi ya wabunge wameipongeza serikali kwa uamuzi huo ambao wamesema utawafanya wananchi wa kigamboni sasa waishi kwa amani lakini pia wameishauri serikali kuliwezesha shirika la nyumba la taifa NHC ili liweze kutekeleza kikamilifu mipango yake ya ujenzi wa nyumba bora na za Gharama nafuu kwa watu wenye kipato cha chini.






No comments: