SIGOMBEI TENA UBUNGE ASEMA ZITTO

Mbunge wa Kigoma kaskazini Mh.Zitto Kabwe ametangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika jimbo hilo baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, huku akiwashukuru wananchi wa jimbo lake kwa kumpa dhamana ya kuwawakilisha bungeni kwa kipindi cha miaka 10 licha ya kukutana na vikwazo vingi.




Akiongea na wapiga kura wake hao Zitto amesema kwa kipindi chote akiwa mbunge alijitahidi kwa kadri alivyoweza kutetea si tu maslahi kwa watu wa jimbo lake bali kwa taifa zima kwa ujumla na kwamba ataendelea kufanya hivyo kama raia ili kuondoa kila aina ya ufisadi na kutumia rasilimali za nchi kuondoa umasikini, ujinga na maradhi.







No comments: