UJENZI WA DAMPO LA KISASA WAKAMILIKA MKOANI MBEYA

Mradi wa ujenzi wa Dampo la Kisasa unaotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la MBEYA kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 3.7 umekamilika tayari , mradi huo utapunguza mlundikano wa taka ngumu na sumu kuzunguka mji wa MBEYA. 







































Afisa Mkuu wa Idara ya Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya SAMWEL BUBEGWA amemwambia Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira Dr BINILITHI MAHENGE kuwa mradi huo unafadhiliwa na benki ya dunia,kinachosubiriwa ni magari ya kubebea taka na vishimba zaidi ya 90 kuwasili kutoka nchini afrika ya kusini. 

Mradi huu unakamilika huku kukiwa na utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais la kufanya usafi wa mazingira kila jumamosi,hata hivyo Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa Rais Mazingira Dokta BINILITHI MAHENGE anawakumbusha wakurugenzi watendaji wa wilaya, miji na majiji kuanza rasmi kutenga bajeti za usafi wa mazingira katika maeneo yao. 







































Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamuu wa Rais mazingira Amehitimisha ziara mkoani Mbeya kwa kugakua kiwanda cha saruji cha Songwe,kilichopo nje kidogo ya Jiji la Mbeya, kiwanda hiki kimekuwa kikilalamikiwa na baadhi ya wananchi juu ya athari za uchafuzi wa mazingira zinazotokana na uzalishaji wa saruji ambalo tatizo kubwa ni vumbi na moshi.













No comments: