WAETHIOPIA 64 WAKAMATWA DODOMA

Jeshi la polisi mkoani Dodoma likishirikiana na wananchi limewakamata wahamiaji haramu 64 raia wa Nchi ya ETHIOPIA (wahebeshi)  katika kijiji cha kidoka kata ya kidoka tarafa ya Goma wilaya ya Chemba mkoani wa Dodoma mmoja kati yao akiwa amefariki alietambuliwa kwa jina moja la TAJIRU  anaekadiriwa kua na umri wa kati ya miaka 25-30 .
                                   Watu hao walikuwa wakisafirishwa kwa Lori lenye namba za usajili T.353 AYW Mitsubishi Fuso lililokuwa likiendeshwa na OTHMAN YUNUS MTEKATEKA, miaka 45, na Mkazi wa ILALA Jangwani  jijini Dar es Salaam akitokea Moshi - Kilimanjaro kwenda mkoani Mbeya.    


              Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma(Pichani juu) Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME – SACP amesema Mnamo tarehe 14/03/2015 saa 01:00 asubuhi katika kijiji cha KIDOKA walionekana watu wengi wasiofahamika wakiwa wamejificha katika vichaka na mashamba ya watu.    




Watu hao walionekana dhaifu, walikuwa wakila mahindi mabichi na wengine wakiomba kwa wanakijiji waliokuwa wakipita maeneo jirani msaada wa chakula na maji ya kunywa kwa ishara,  kwa kuwa hawakuwa na uwezo wa kuongea lugha ya Kiingereza wala Kiswahili. 































































No comments: