ZITO BADO NI MBUNGE HALALI WA KIGOMA KASKAZINI ASEMA MAKINDA

Spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania  Mhe.Anna Makinda amesema Zitto Zubeir Kabwe bado ni mbunge halali wa jimbo la Kigoma kaskazini kutokana na spika huyo kutokupata taarifa rasmi kutoka tume ya taifa ya uchaguzi  kuhusiana na kutengeliwa ubunge huo.
 




















Makinda alitoa kauli hiyo kwenye  mkutano wa kumi na tisa wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania ambao umeanza leo mkoani Dodoma huku serikali ikisema madhaifu yaliyopo katika jeshi la polisi yamechangia vitendo vya uporaji na uvamizi wa vituo vya polisi.




Dakika chache baada ya mkutano huo kuanza spika wa bunge 
Mhe.Anna Makinda aliwataka wabunge wasimame kimya dakika moja kumkumbuka aliyekuwa mbunge wa jimbo la mbinga magharibi kapteni mstaafu John Komba aliyefariki hivi karibuni



Katika kipindi cha maswali na majibu, naibu waziri wa mambo ya ndani Pereira Sillima amesema madhaifu yaliyopo kwa baadhi ya askari polisi yamekuwa yakichangia vituo hivyo kuvamiwa na polisi kuporwa silaha hivyo ni bora polisi wakajirekebisha.



No comments: