Serikali imekubali kufuta utaratibu
wa kuwataka madereva kusoma upya kwenye chuo cha taifa cha usafirishaji (NIT)
mara tu baada ya kuisha kwa muda wa leseni zao
waziri wa kazi na ajira Mh Gaudencia Kabaka
Akizungumza na baadhi ya madereva kwenye
stendi kuu ya mabasi
yaendayo mikoani (Ubungo) mara baada ya kumalizika kwa
kikao kilichowahusisha madereva, wamiliki wa mabasi pamoja na serikali
kilichofanyika Ubungo waziri wa kazi na ajira Mh Gaudencia Kabaka alisema kuwa
serikali imekubali kufuta utaratibu huo wakuwataka madereva kwenda kusoma kila
baada ya leseni zao kuisha muda wake.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya
madereva kutoka maeneo mbalimbali nchini kugoma na kuishinikiza serikali kuondoa
utaratibu wa kuwataka madereva kuanza kusoma baada ya leseni zao kuisha muda
wake na kutaka kuwekewa mazingira mazuri kwenye kazi yao.
Nae kwa upande wake kamanda wa polisi
kanda maalumu ya Dar es salaam Kamishina Suleimani Kova wakati akizungumza na
madereva hao aliwaahidi kuwa ataondoa utarati wa kuweka vipima spidi maarufu
kama Tochi kwenye maeneo mbalimbali ambayo nayo nimoja ya kero kwa madereva
hao.
Uamuzi wa serekali umefanya hali ya
usafiri kurudi katika hali ya kawaida mara baada ya madereva kukubali kusitishi
mgomo na kuendelea na kazi kama kawaida.
No comments:
Post a Comment