KIKEKE, ALI KIBA, MILLARD AYO WANG'ARA "TUZO ZA WATU" 2015

Mtangazaji maarufu wa kipindi cha dira ya dunia kinachorushwa na idhaa ya kiswahili ya bbc London salim kikeke ameibuka mshindi katika kategori ya mtangazaji wa luninga anaependwa zaidi katika tuzo za watu kwa mwaka 2015.

Katika hafla ya ugawaji wa tuzo hizo iliyofanyika jana kikeke aliwashinda watangazaji mbalimbali aliokuwepo nao kwenye kategori hiyo ambao ni salama jabir, Dulla ambua na Sam misago wa east Africa TV pamoja na zamaradi mketema wa clouds tv.

Katika hatua nyingine mtangazaji wa clouds fm Millard ayo amechukua tuzo ya blogu/tovuti inayopendwa zaidi kupitia tovuti yake ya Millard ayo.com akizishinda blogu na tovuti nyingine kama michuzi blog zilizokuwepo kwenye kategori hiyo.

Kwa upande wa  wasanii msanii wa kizazi kipya Ali kiba amechukua tuzo ya msanii wa kiume anaependwa zaidi huku kwa upande wa wanawake tuzo hiyo ikienda kwa msanii lady jaydee.

Hivi ni vipengele vyote pamoja na washindi wa tuzo hizo

Mtangazaji wa redio anaependwa
D' jaro arungu TBC FM

Kipindi cha redio kinachopendwa
Papaso  TBC FM

Mtangazaji wa runinga anaependwa
Salim kikeke BBC SWAHILI

Kipindi cha runinga kinachopendwa
Mkasi EATV

Blogu/ tovuti inayopendwa
Millard ago.com

Muongozaji video anaependwa
Hasscana.

Muongozaji filamu anaependwa
Rey kigosi

Muigizaji filamu wa kike anaependwa wema sepetu

Muigizaji filamu wa kiume anaependwa
Hemedy PhD

Msanii wa muziki wa kiume anaependwa
Ally kiba

Msanii wa muziki wa kike anaependwa
Lady jaydee

Filamu inayopendwa
Kigodoro

Video ya muziki inayopendwa
Nani kama mama
Christian bella ft Omy dimpozi.







No comments: